Kama tunavyojua shetani ni
muwindaji hivyo huweka mitego kutunasa .Na mitego hii haiwi wazi wazi na
hulenga sehemu ambayo ni rahisi kuwanasa watu wengi kwa hila.
2Timotheo 2;26.wapate tena fahamu zao nakutoka katika mtigo
wa ibilisi
Miongoni mwa vitu vilivyoibuka Tanzania na duniani kwa ujumla
makanisani yamekuwa mitego.Nayo ni SACCOS NA RIBA makanisani.Na makanisa
mengine yako mbioni kuanzisha BENKI na SACCOS.Je tunakumbuka Yesu alivyosema
nyumba yangu mmegeuza kuwa nyumba ya biashara? .Yohana 2;13-16…..msiifanye nyumba ya baba yangu kuwa nyumba ya biashara.......
Benki na SACCOS inaendesha biashara
kwa kudai riba .Riba ni mtego mkubwa sana katika ukristo.
Sasa Je mtu aliyeokoka anaweza kumkopesha mtu na kudai kurudishiwa riba?
Riba ni kiasi cha ziada nje na mkopo wenyewe.
Rehani ni kile kitu kilichotolewa kama fidia kwakushindwa
kulipa mkopo.
REHANI.
Kama mtu
ameshindwa kurudisha mkopo ukataka kuchukua rehani kwa mujibu wa maandiko matakatifu
huruhusiwi kumchukua au kumnyang’anya kitu chochote ila unatakiwa mdaiwa
achague mwenyewe anachotoa.Kumbukumbu
24;10-13,..umkopeshapo jirani jirani
yako chochote kikopeshwacho usiingie nyumbani mwake kutwa rehani
kwake...........
Kama mdaiwa
ni maskini hutakiwi kuchukua kitu muhimu kwake mfano nguo,chakula nk ila kwa
idhini yake atatoa chochote kama rehani
.Kutoka 22;26-27........
Kama mtu ni
mjane ni mwiko kabisa kuchukua nguo zake kama rehani au ng’ombe wake..Kumbukumbu 24;17-18.Ayubu 24;2,3b,9b.
Maskini
ndio hao wanao chukua mikopo na wengine ni wajane je kanisa litakwepa vipi
katika utoaji wa mikopo na rehani tena bila upendeleo?
Kitu ambacho ni uhai au la kijisitiri
huruhusiwi kutochukua kama rehani.Au na mna yyoyote ya kumkosesha mtu kula au
riziki ni kosa tena biblia imelifananisha na jiwe la kusagia ukichukua jiwe
lolote kati ya yale mawili la juu au la chini ni kosa kwasababu utakuwa
umemkosesha kula.
Unatakiwa
uwe na moyo wa kusaidia na sio kutafuta faida.Kumbukumbu 24;6-10.
Hatuwezi
kuchukua shamba la mtu au mizabibu kwa rehani.Nehemia alikasirishwa sana na
hilo .Nehemia 1;1-4 ndugu
linamaanisha waliookolewa kwani baba yetu ni mmoja.Warumi 16;14,1;1.Mathayo 18;15-17.Miili yetu kama yao maana yake
nao wanakula kama sisi wanategemea mashamba na chakula.
RIBA
Kama
unamkopesha ndugu yako(aliyeokoka) hautakiwi kumdai riba ila kwa watu wa
mataifa(ambao hawajaokoka)Kumbukumbu
23;19-20. Walawi 25;35=38’Nehemia 5;1-6,5;7-10.Nehemia alikasirishwa sana
kwa habari ya riba.
Sifa za
atakaye ingia mbinguni Zaburi 15;1-5”hakutoa
fedha yake kula riba”Nyakati hizi watu watapernda fedha tuwe makini.2Timotheo 3;2
No comments:
Post a Comment