Thursday, November 15, 2012

RIBA NA REHANI KATIKA UKRISTO.



Kama tunavyojua shetani ni muwindaji hivyo huweka mitego kutunasa .Na mitego hii haiwi wazi wazi na hulenga sehemu ambayo ni rahisi kuwanasa watu wengi kwa hila.
2Timotheo 2;26.wapate tena fahamu zao nakutoka katika mtigo wa ibilisi

Miongoni mwa vitu vilivyoibuka Tanzania na duniani kwa ujumla makanisani yamekuwa mitego.Nayo ni SACCOS NA RIBA makanisani.Na makanisa mengine yako mbioni kuanzisha BENKI na SACCOS.Je tunakumbuka Yesu alivyosema nyumba yangu mmegeuza kuwa nyumba ya biashara? .Yohana 2;13-16…..msiifanye nyumba ya baba yangu kuwa nyumba ya biashara.......
         Benki na SACCOS inaendesha biashara kwa kudai riba .Riba ni mtego mkubwa sana katika ukristo.
       
Sasa Je mtu aliyeokoka anaweza kumkopesha mtu  na kudai kurudishiwa riba?                    
Riba ni kiasi cha ziada nje na mkopo wenyewe.
Rehani ni kile kitu kilichotolewa kama fidia kwakushindwa kulipa mkopo.

REHANI.
Kama mtu ameshindwa kurudisha mkopo ukataka kuchukua rehani kwa mujibu wa maandiko matakatifu huruhusiwi kumchukua au kumnyang’anya kitu chochote ila unatakiwa mdaiwa achague mwenyewe anachotoa.Kumbukumbu 24;10-13,..umkopeshapo jirani jirani yako chochote kikopeshwacho usiingie nyumbani mwake kutwa rehani kwake...........

Kama mdaiwa ni maskini hutakiwi kuchukua kitu muhimu kwake mfano nguo,chakula nk ila kwa idhini yake atatoa chochote kama rehani
.Kutoka 22;26-27........

Kama mtu ni mjane ni mwiko kabisa kuchukua nguo zake kama rehani au ng’ombe wake..Kumbukumbu 24;17-18.Ayubu 24;2,3b,9b.
Maskini ndio hao wanao chukua mikopo na wengine ni wajane je kanisa litakwepa vipi katika utoaji wa mikopo na rehani tena bila upendeleo?
     Kitu ambacho ni uhai au la kijisitiri huruhusiwi kutochukua kama rehani.Au na mna yyoyote ya kumkosesha mtu kula au riziki ni kosa tena biblia imelifananisha na jiwe la kusagia ukichukua jiwe lolote kati ya yale mawili la juu au la chini ni kosa kwasababu utakuwa umemkosesha kula.

Unatakiwa uwe na moyo wa kusaidia na sio kutafuta faida.Kumbukumbu 24;6-10.
Hatuwezi kuchukua shamba la mtu au mizabibu kwa rehani.Nehemia alikasirishwa sana na hilo .Nehemia 1;1-4 ndugu linamaanisha waliookolewa kwani baba yetu ni mmoja.Warumi 16;14,1;1.Mathayo 18;15-17.Miili yetu kama yao maana yake nao wanakula kama sisi wanategemea mashamba na chakula.

RIBA
Kama unamkopesha ndugu yako(aliyeokoka) hautakiwi kumdai riba ila kwa watu wa mataifa(ambao hawajaokoka)Kumbukumbu 23;19-20. Walawi 25;35=38’Nehemia 5;1-6,5;7-10.Nehemia alikasirishwa sana kwa habari ya riba.

Sifa za atakaye ingia mbinguni Zaburi 15;1-5”hakutoa fedha yake kula riba”Nyakati hizi watu watapernda fedha tuwe makini.2Timotheo 3;2

No comments:

Post a Comment