Tuesday, November 6, 2012

Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

JF Focus: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)
By Mwali
Swali la kwanza:

Rais Kikwete amekuwa madarakani tokea mwaka 2005. Ukilinganisha na utawala wa Marais wastaafu, Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi na Mkapa, nini maoni yako kuhusiana na utawala Rais Kikwete? Rais Kikwete ana yapi ya kujivunia aliyofanya katika kipindi cha miaka aliyokaa madarakani? Jibu la swali liguse sekta zote kuanzia ya uchumi, afya, usafiri,sheria na utawala, michezo, n.k.

Una dakika kumi kujibu swali hili, kisha hapo nitamwelekeza Matola.
Kwanza kabisa napenda kuelezea kuwa nimefurahi sana kuwa swali limelenga moja kwa moja kwenye kulinganisha madaraka ya Rais wa sasa mpendwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete na awamu zilizopita za “Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi na Mkapa”. Kama swali linavyojionesha “ana yapi ya kujivunia aliyofanya katika kipindi cha miaka aliyokaa madarakani?” katika nyanja tofauti, hususan “uchumi, afya, usafiri, sheria na utawala, michezo, n.k.”

Napenda kuainisha majibu yagu ya awali na kuwajulisha wasimamizi na wafatiliaji mnakasha huu huu, kuwa kila nyanja imesheheni nakshi na fasaha na tawimu teletele, kweny "post" hii ntaanza na moja la "uchumi" na post zifuatazo ntawasilisha yanayohusu mengineyo kama yalivyo kwenye swali:

Uchumi wakati wa Nyerere;

Ikumbukwe kuwa, wakati Mwalim Nyerere anapewa madaraka ya nchi hii uchumi wa Tanganyia ulikuwa mzuri sana hususan katika kilimo, Tanganyika ilikuwa ni muuzaji mkubwa wa mazao nje ya Tanganyika katika Afrika, Nyerere kwa muda mfupi tu akatutoa huko na kutufikisha kuwa waagiizaji wakibwa wa chakula.
Under his Presidency, Tanzania slipped from being the largest exporter of food in Africa to the biggest importer of food.

Source: Mwalimu Nyerere | Julius Nyerere; Life Times Legacy

Tanzania slipped from being the largest exporter of food in Africa to the biggest importer of food.

Source: Julius Nyerere - New World Encyclopedia

Kwa kifupi kwa kuwa hatumzungumzii Nyerere, na “sources” zipo nyingi sana zinazoonesha jinsi uchumi wetu ulivyoporomoka sana wakati wake, naomba atakae a google “economy collapsed during Nyerere” atajionea mwenyewe maana nikianza kuyabandika hapa tutatoka nje ya mnakasha.Kwa kifupi, hatuna cha kujivunia katika uchumi wakati wa Nyerere tuliushuhudia ukiporomoka kwa kujaribu kwake kufata mfumo wa ujamaa ambao ulishindwa kabisa.

Uchumi wakati wa Mwinyi;

Ikumbukwe kwamba Mwinyi ndiye alikuwa “savior” wa waTanzania mpaka akapewa jina la “Ruksa” kwa sababu ni yeye aliyetufungulia milango ya uchumi huria ni yeye aliyeleta maamuzi ya kufunga mashirika ya umma yaliyokuwa yananyonya uchumi wote wa Tanzania kwa kupewa ruzuku hata yanapofanya vibaya. Kwa kifupi Mzee Mwinyi alikuwa na kazi ngumu sana ya kutuondoa kwenye lindi la umaskini na kutuanzishia mfumo mpya wa uchumi ambao tunaendelea nao. Kwa hilo tumsifu Mzee Mwinyi:

During Mwinyi's terms Tanzania took the first steps to reverse the socialist policies of Julius Nyerere. [2] He relaxed import restrictions and encouraged private enterprise.

Soma zaidi: Ali Hassan Mwinyi - Wikipedia, the free encyclopedia

In 1986 the newly-appointed Mwinyi Government embarked on a broad-based Economic Recovery Program supported by the International Monetary Fund (IMF) and the World Bank. This was reinforced by an Economic and Social Action Program in 1989. Under these two programs, Government worked to dismantle the system of state controls and promote private sector expansion--including liberalizing the trade and exchange system, eliminating price controls and most state monopolies, and opening the financial sector to private sector participation. Rehabilitation of key infrastructure was also made a priority, particularly roads, railways, and ports.

Source: Foodnet-Uganda > Market Information

Uchumi wakati wa Mkapa;

Mkapa kwenye uchumi aliendeleza aliyoyanzisha Mwinyi nae akatia mkazo kwenye kukaribisha wageni kuwekeza tukaona “influx” ya makampuni makubwa ya kigeni yakipewa vitalu vya uwindaji, ardhi kubwa za kuchimba madini, Ulikuwa ni muelekeo mzuri kiuchumi kinadharia.

Kosa kubwa nilionalo ni pale “corruption” ya hali ya juu ilipokithiri wakati wa Mkapa, hususan baada ya kifo cha Nyerere. Madudu wmengi au karibu yote yanayoibuka sasa utakuta yameanzia au yemetendeka wakati wa Mkapa; EPA, KIWIRA, BOT, RADAR, kuainisha machache. Sina mengi ya kumsifu kwani kipindi chake cha mwisho aliharibu sana kwa kutuacha Kiza na kwa tuhuma nyingi za ufisadi zilizodhihirika “immediately” baada ya kuondoka kwake madarakani na mpaka leo bado zinatutesa.

Uchumi wakati wa Kiwete;

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ana kila sababu za kujivunia katika uchumi wakati wa madaraka yake, kwa uchache kuhusu uchumi ni haya hapa yakiambatana na takwimu zilizo wazi kabisa:

Asalaam Aleykum,

kwanza nawapongeza kwa mara nyingine tena wale wote ambao wako kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, nawapongeza na wale wengine wote wasiopo kwenye mfungo lakini wanauheshimu mwezi huu, wanaheshimu uamuzi wetu wakufunga na tunawashukuru zaidi kwa kutupa hamasa sisi tulio kwenye swaum.

Natamani kuingia moja kwa moja kwenye kujibu swali la kwanza, lakini uungwana hauniachi kufanya hivyo bali unanilazimisha kutoa pongezi zangu za dhati kwa walioubuni mnakasha huu. Natoa shukrani zangu pia kwa mshiriki mwenzangu wa mnakasha huu al maaruf Matola kwa kukubali kushiriki, halikadhalika natoa shukrani zangu kwa wote waliojitolea kuufatilia mnakasha huu.

Naanza:

Kwanza kabisa napenda kuelezea kuwa nimefurahi sana kuwa swali limelenga moja kwa moja kwenye kulinganisha madaraka ya Rais wa sasa mpendwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete na awamu zilizopita za “Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi na Mkapa”. Kama swali linavyojionesha “ana yapi ya kujivunia aliyofanya katika kipindi cha miaka aliyokaa madarakani?” katika nyanja tofauti, hususan “uchumi, afya, usafiri, sheria na utawala, michezo, n.k.”

Napenda kuainisha majibu yagu ya awali kuyapanga kama yalivyo:

Uchumi wakati wa Nyerere;

Ikumbukwe kuwa, wakati Mwalim Nyerere anapewa madaraka ya nchi hii uchumi wa Tanganyia ulikuwa mzuri sana hususan katika kilimo, Tanganyika ilikuwa ni muuzaji mkubwa wa mazao nje ya Tanganyika katika Afrika, Nyerere kwa muda mfupi tu akatutoa huko na kutufikisha kuwa waagiizaji wakibwa wa chakula.

Under his Presidency, Tanzania slipped from being the largest exporter of food in Africa to the biggest importer of food.

Source: Mwalimu Nyerere | Julius Nyerere; Life Times Legacy

Tanzania slipped from being the largest exporter of food in Africa to the biggest importer of food.

Source: Julius Nyerere - New World Encyclopedia

Kwa kifupi kwa kuwa hatumzungumzii Nyerere, na “sources” zipo nyingi sana zinazoonesha jinsi uchumi wetu ulivyoporomoka sana wakati wake, naomba atakae a google “economy collapsed during Nyerere” atajionea mwenyewe maana nikianza kuyabandika hapa tutatoka nje ya mnakasha.

Kwa kifupi, hatuna cha kujivunia katika uchumi wakati wa Nyerere tuliushuhudia ukiporomoka kwa kujaribu kwake kufata mfumo wa ujamaa ambao ulishindwa kabisa.

Uchumi wakati wa Mwinyi;

Ikumbukwe kwamba Mwinyi ndiye alikuwa “savior” wa waTanzania mpaka akapewa jina la “Ruksa” kwa sababu ni yeye aliyetufungulia milango ya uchumi huria ni yeye aliyeleta maamuzi ya kufunga mashirika ya umma yaliyokuwa yananyonya uchumi wote wa Tanzania kwa kupewa ruzuku hata yanapofanya vibaya.

Kwa kifupi Mzee Mwinyi alikuwa na kazi ngumu sana ya kutuondoa kwenye lindi la umaskini na kutuanzishia mfumo mpya wa uchumi ambao tunaendelea nao. Kwa hilo tumsifu Mzee Mwinyi:

During Mwinyi's terms Tanzania took the first steps to reverse the socialist policies of Julius Nyerere. [2] He relaxed import restrictions and encouraged private enterprise.

Soma zaidi: Ali Hassan Mwinyi - Wikipedia, the free encyclopedia

In 1986 the newly-appointed Mwinyi Government embarked on a broad-based Economic Recovery Program supported by the International Monetary Fund (IMF) and the World Bank. This was reinforced by an Economic and Social Action Program in 1989. Under these two programs, Government worked to dismantle the system of state controls and promote private sector expansion--including liberalizing the trade and exchange system, eliminating price controls and most state monopolies, and opening the financial sector to private sector participation. Rehabilitation of key infrastructure was also made a priority, particularly roads, railways, and ports.

Source: Foodnet-Uganda > Market Information

Uchumi wakati wa Mkapa;

Mkapa kwenye uchumi aliendeleza aliyoyanzisha Mwinyi nae akatia mkazo kwenye kukaribisha wageni kuwekeza tukaona “influx” ya makampuni makubwa ya kigeni yakipewa vitalu vya uwindaji, ardhi kubwa za kuchimba madini, Ulikuwa ni muelekeo mzuri kiuchumi kinadharia.

Kosa kubwa nilionalo ni pale “corruption” ya hali ya juu ilipokithiri wakati wa Mkapa, hususan baada ya kifo cha Nyerere. Madudu wmengi au karibu yote yanayoibuka sasa utakuta yameanzia au yemetendeka wakati wa Mkapa; EPA, KIWIRA, BOT, RADAR, kuainisha machache. Sina mengi ya kumsifu kwani kipindi chake cha mwisho aliharibu sana kwa kutuacha Kiza na kwa tuhuma nyingi za ufisadi zilizodhihirika “immediately” baada ya kuondoka kwake madarakani na mpaka leo bado zinatutesa.

Uchumi wakati wa Kiwete;

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ana kila sababu za kujivunia katika uchumi wakati wa madaraka yake, nnadiriki kusema kuwa hakuna nyanja ambayo Kikwete hajavunja rikodi zilopo kabla yake katika kuyatimiza. Kwa uchache kuhusu uchumi ni haya hapa yakiambatana na takwimu zilizo wazi kabisa:

1. USIMAMIZI WA UCHUMI JUMLA:

Ukuaji wa Uchumi Katika kipindi cha miaka minne (2005 – 2009). Uchumi umeendelea kuimarika na Pato la Taifa lilikua kwa wastani wa asilimia 7.2 kwa mwaka katika kipindi hicho. Ukuaji huu wa uchumi ulichangiwa zaidi na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi katika sekta za: Bidhaa za viwanda; ujenzi; fedha; na mawasiliano na uchukuzi.

2. PATO LA MTANZANIA;

Pato la Mtanzania limekuwa likiongezeka katika kipindi chote cha awamu ya nne kutoka Dola za Kimarekani 392.8 mwaka 2005 hadi dola 525.2 mwaka 2008.

3.MWENENDO WA RIBA;

Viwango vya riba vimeonesha mwelekeo mzuri hasa kuanzia mwaka wa fedha 2006/07, ambapo riba kwenye amana za akiba zimekuwa zikiongezeka, wakati riba zinazotozwa kwenye mikopo zimekuwa zikipungua. Katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka 2009/10 wastani wa viwango vya riba kwa amana za akiba za muda mfupi (hadi mwaka mmoja)ulikuwa asilimia 8.92 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 5.21 katika mwaka wa fedha 2003/04.

Katika kipindi hicho, wastani wa viwango vya riba vilivyotozwa na benki za biashara kwa mikopo ya mwaka mmoja ulipungua hadi asilimia 13.93 kutoka asilimia 15.75. Kutokana na mwelekeo huo wa riba, tofauti kati ya viwango vya riba kwenye amana za mwaka mmoja na viwango vya riba kwenye mikopo ya mwaka mmoja ilishuka kutoka 10.54 mwaka 2003/04 hadi 5.01mwaka 2009/10, sawa na kushuka kwa asilimia 47.5.

4. BIASHARA YA BIDHAA NJE;

Mauzo ya bidhaa nje yaliongezeka kwa asilimia 3.2 hadi kufikia dola za Kimarekani 2,697.6 milioni mwezi Novemba 2009. Ongezeko hilo lilichangiwa na mauzo ya dhahabu kwa asilimia 9.0 hadi kufikia dola 1,023.8 milioni, tumbaku kwa asilimia 35.3 hadi kufikia dola 151.4. Aidha, mauzo ya kahawa nje yaliongezeka hadi kufikia dola 117.2 milioni, sawa na asilimia 29.0.

5.MAPATO YA NDANI;

Katika kipindi cha miaka minne, Wizara ya Fedha na Uchumi, kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imefanya marekebisho ya mifumo na viwango vya baadhi ya kodi. Hatua hii imesaidia kuweka mazingira mazuri zaidi ya uzalishaji kurahisisha ukusanyaji wa kodi. Aidha, wigo wa kodi umeongezeka katika kipindi hicho.

6.KUWEZESHA UPATIKANAJI WA MIKOPO;

Mikopo iliyotolewa na mabenki kwa sekta binafsi kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi iliongezeka kutoka shilingi bilioni 1,571.0 mwezi Desemba 2005 hadi shilingi bilioni 4,710.2 mwezi Juni 2009, sawa na ongezeko la wastani wa asilimia 34.5 kwa mwaka. Mwezi Oktoba 2009 mikopo hiyo ilikuwa imefikia shilingi bilioni 4,836.0. Aidha, wastani wa riba kwa dhamana zote ilishuka kutoka asilimia 16.4,

7.KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI;

Mifuko ya Dhamana ya Mikopo (Credit Guarantee Scheme): Kuanzishwa kwa Mfuko wa Dhamana wa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME Credit Guarantee Scheme) ambao unaratibiwa na Benki Kuu kumeboresha mazingira ya wenye mitaji midogo na ya kati waweze kupatamikopo kutoka kwenye mabenki na taasisi za fedha. Tangu mfuko huu uanzishwe, jumla ya SMEs 48 zimepata udhamini wa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 3.054. Kati ya wajasiliamali hao, sekta ya uzalishiji inaongoza ikifuatiwa na sekta za ujenzi na kilimo. Ili kuleta ufanisi zaidi, mwaka huu Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni 10 kuongeza mtaji wa mfuko wa wajasiliamali wadogo na wa kati.

Kuongeza fedha katika Mfuko wa Uwezeshaji Kiuchumi wa wajasiriamali wadogo (Mfuko wa JK) kiasi cha Shilingi bilioni 10.5 kupitia benki ya NMB. ilitoa kiasi cha Shilingi bilioni 10.5 kupitia benki ya NMB (Shilingi bilioni 5.25) na CRDB (Shilingi bilioni 5.25). Kiasi hiki kiliwezesha kutolewa kwa mikopo ya Shilingi bilioni 37.17 ikiwa in asilimia 118 ya Shilingi 31.5 zilizotengwa kutolewa na benk hizo mbili.

Hayo ni baadhi tu ya mafanikio ya kujivunia ya kiuchumi Tanzania na yapo mengi sana, kuanzia mabarabara ya nayoendelea kujegwa hivi sasa, mitambo ya uzalishaji umeme inayoendelea kujengwa hivi sasa, kiwanda kikubwa cha chuma kinachoendelea kujengwa hivi sasa.

Licha ya hayo kuna msukumo ulifanyawa na Kikwete wa makusudi kabisa katika kuendeleza sekata ya mali asili na katika kipindi chake tumeona makampuni makubwa duniani yakivumbuwa gas ya asili kwa kiwango kikubwa sana na hili ni jema sana katika uchumi wetu wa siku za usoni. Hapa nnadiriki kusema kuwa wa kabla yake "uchumi walikuwa nao lakini waliukalia", Kikwete kabadili hilo badili ya kuukalia kausimamia kidete na matokeo hakuna asiyeyajuwa, Tanzania economy inabadilika kutoka kilimo kuwa namba moja kwenda kwenye Gas ya asili.

Hapo nimegusa uchumi tu, dakika kumi hazitoshi kuelezea mengi mema ya Kikwete.

No comments:

Post a Comment